Pages

Wednesday, June 27, 2012

Hivi ndivyo alivyokutwa Dr.Ulimboka










Kwa mujibu wa mtandao wa Jamii Forums Dr. Ulimboka ametekwa majira ya saa sita usiku na watu watatu waliokuwa na silaha za moto na kumpeleka kusikojulikana! Inasemekana alipigiwa simu na jamaa mmoja aliyejitambulisha kwa jina moja la 'Abeid' ambaye tangu mwanzo amekuwa akiwasiliana naye na kujiita afisa wa serikali na kudai kuwa alitaka aonane naye face to face kwa ajili ya mazungumzo.

Dokta huyo aliokotwa akiwa na hali mbaya sana na hawezi kuzungumza.

Tukio hilo limetokea wakati kumekuwepo na mgomo wa madaktari nchi nzima ambao hata hivyo wameonekana kusalitiana kwa kutokuwa na msimamo wa pamoja, kwani maeneo mengine yote huduma zimeendelea kama kawaida, isipokuwa katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili.

Madaktari hao wametangaza mgomo usio na kikomo kwa lengo la kuishinikiza serikali kutimiza mahitaji yao, ikiwemo kuboresha mazingira ya kufanyia kazi pamoja na kuwapandishia mishahara.

Licha ya mgomo huo kuanza kuleta madhara kwa wagonjwa katika siku ya kwanza juzi, kwa madaktari kutofanya kazi katika hospitali mbalimbali nchini, jana hali hiyo ilikuwa tofauti kwani sehemu nyingi huduma ziliendelea kutolewa kama kawaida.
SOURCE THIS DAY MAGAZINE




Wednesday, June 6, 2012

Cheki picha za Millard na Hasheem alafu uangalie pia na picha za Millard na Linah,,Pata picha itakuje Linah akisimama na Hasheem Thabeet

http://millardayo.com/wp-content/uploads/2012/06/Millard-Ayo-Linah.jpg
Millard and Linah
http://millardayo.com/wp-content/uploads/2012/06/310.jpg
Millard an Hasheem
http://millardayo.com/wp-content/uploads/2012/06/116.jpg
Millard and Hasheem
http://millardayo.com/wp-content/uploads/2012/06/Millard-Ayo-na-Linah-1.jpg
Millard and Linah 







VIONGOZIN WA UAMSHO WAZIDI KUJISALIMISHA POLISIN ZAZIBAR

VIONGOZIN WA UAMSHO WAZIDI KUJISALIMISHA POLISIN ZAZIBAR


ZANZIBAR JUMANNE JUNI 4, 2012. VIONGOZI wengine wawili wa Jumuiya ya Uamsho Visiwani Zanzibar, leo wamefika Makao Makuu ya Upelelezi Zanzibar ambako walihojiwa kwa muda kuhusiana na vurugu za wiki iliyopita visiwani hapa kabla ya kuachiliwa.
Inspekta Jenerali wa Polisi (IGP), Said Mwema

Afisa Habari Mkuu wa Jeshi la Polisi Zanzibar Inspekta Mohammed Mhina, amewataja Viongozi waliofika Polisi na kuhojiwa kuwa ni Mwenyekiti wa Jumuiya ya Uamshio Shekhe Mselem Bin Ali, mkazi wa Makadara na Shekhe Azan Ahmed Saidi, wa Mfenesini.
Inspekta Mhina amesema katika mahojiano hayo Polisi walibaini kuwa siku ya vurugu hizo, viongozi hao hawakuwepo mjini Zanzibar ingawa Polisi walitaka kujua zaidi kama wao walihusika katika maandalizi ya awali ya mpango huo kabla ya kuondoka kisiwani hapa.
Wakati wa matukio hayo Sheikhe Mselem alikuwa Pemba na Shekhe Azan alikuwa Uwarabuni kwa matibabu lakini alilazimika kurejea Zanzibar baada ya kusikia hali ya vurugu zilizofanywa na vijana wa kikundi chake.
Viongozi hao wanafanya idadi ya viongozi waandamizi wa Jumuiya hiyo waliojisalimisha na kuhojiwa kwa hiyari na Makachero wa Jeshi la Polisi mjini Zanzibar kufikia sita.
Jana viongozi wengine wanne kutoka katika kundi hilo la Uamsho, walijisalimisha wenyewe Polisi na kuhojiwa kwa masaa kadhaa kabla ya kuachiwa kwa masharti.
Inspekta Mhina amesema kuwa bado Jeshi la Polisi linaendelea kutoa wito kwa viongozi wengine wa Jumuiya hiyo ambao hawajafika Polisi, kufanya hivyo badala ya kusakwa na kutiwa nguvuni kuhusiana na vurugu hizo.
Wiki iliyopita Waziri wa Mambo ya Ndani Mh. Emmanuel Nchimbi na Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini Inspekta Jenerali Saidi Mwema, walifika mjini Zanzibar na kuwataka wale wote waliohusika katika vurugu hizo kujitokeza kukabili mkono wa sheria.
Tayari watu 78 wamekamatwa na Polisi na kufikishwa mahakamani kwa tuhuma za kufanya vurugu zilizosababisha kuchomwa moto kwa magari na baadhi ya makanisa mjini Zanzibar.
Imeandaliwa na Mwandishi wa Jeshi la Polisi, Zanzibar

Polisi wapora maiti walioua kwa risasi mgodini Tarime





Polisi wapora maiti walioua kwa risasi mgodini Tarime

JESHI la Polisi Kanda Maalumu ya Tarime na Rorya Mkoani Mara, kupitia askari wake wa FFU limelazimika kutumia nguvu pamoja na kuwatisha kwa silaha wananchi na waombolezaji wa marehemu, Mgosi Magasi Chacha (30), aliyekufa baada ya kupigwa risasi ya moto na polisi wanaolinda mgodi wa North Mara uliopo Wilayani hapa.
Sehemu ya mgodi wa dhahabu wa North Mara, unaomilikiwa na African Barrick Golds
Katika tukio hilo la jana Jumanne saa 5:10 asubuhi, polisi wakiwa kwenye magari manne huku wakiwa wamebeba silaha ikiwamo bunduki aina ya SMG, mabomu ya machozi na marungu, waliwasili kwenye hospitali ya wilaya ya Tarime kuchukuwa mwili wa marehemu Chacha kwa nguvu ili kwenda kuuzika baada ya kuwakamata baadhi ya viongozi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) waliokuwa katika msiba huo.
Mgodi wa North Mara unamilikiwa na kampuni kubwa ya uchimbaji madini duniani ya Barrick Gold, na umekuwa katika mgogoro na wenyeji wa eneo hilo mara kwa mara hali inayosababisha kuwapo kwa matukio yanayohatarisha amani mara kwa mara.
Wakati polisi hao wa FFU waliokuwa wametanda aneo kubwa la hospitali hiyo wakitaka kuchukua mwili wa marehemu, mamia ya wananchi, ndugu wa marehemu akiwemo mkewe (jina lake halikupatikana), pamoja na viongozi wa Chadema wilaya ya Tarime, waliwazuia polisi kuuchukuwa mwili huo, wakitaka lazima taratibu za kisheria zifuatwe na si vinginevyo.
Baada ya viongozi hao wa Chadema, wananchi, ndugu na jamaa wa marehemu Chacha kuchachamaa, mke wa marehemu alikuwa akilia kwa uchungu huku akiwa amekaa karibu na mlango wa chumba cha kuhifadhia maiti, akikataa polisi kuchukuliwa mwili wa mumewe kwenda kuuzika bila ndugu na yeye kuridhia, lakini askari kanzu mmoja wa kiume alionekana kuanza kumburuza mke huyo wa marehemu kwa lengo la kumtoa eneo hilo ili polisi wachukuwe mwili huo.
Wakati mke huyo wa marehemu akiburuzwa na mmoja wa askari polisi aliyekuwa akitii amri ya mkubwa wake wa kazi (majina hayakupatikana), mwanamke huyo alikataa katakata kuondoka, lakini polisi nao walionekana kumlazimisha hadi baadhi ya nguo zake alizokuwa amejifunga zikidondoka kisha baadhi ya maeneo ya mwili wake juu ya kiuno yakiwa yanaonekana nje, jambo ambalo lilioelezwa na walioshuhudia  kama ni udhalilishaji.
Mwandishi wa habari hizi alishuhudia vurugu hizo, baina ya polisi na ndugu wa marehemu, ambapo polisi walilazimika kuweka chemba risasi za moto katika bunduki zao za SMG, baada ya kuona wametaka kuzidiwa nguvu, ambapo waliwakamata na kuwaweka ndani mwenyekiti wa Chadema wilayani Tarime, Lucas Ngoto.
Viongozi wengine wa Chadema waliokamatwa na polisi katika tukio hilo ni, Katibu wa Chadema wilaya hiyo, Mroni Mwita pamoja na diwani wa Kata ya Sabasaba, Christopher Chometa, huku mwenyekiti wa Baraza la Vijana Chadema (Bavicha), wilaya ya Tarime, Chacha Heche akiponea chupuchupu kukamatwa kwa madai ya kutaka kuzuia mwili huo wa marehemu usiondolewe hospitalini hapo kwenda kuzikwa.
Marehemu Chacha mkazi wa Kijiji cha Nkende ambaye alikuwa mwendesha pikipiki wilayani Tarime, aliuawa Juni 4 mwaka huu majira ya saa 1:45 asubuhi, kwa kupigwa risasi ubavuni kisha kutokea tumboni na askari polisi wanaolinda mgodi huo wa North Mara, unaomilikiwa na kampuni ya Barrick, na kwamba jeshi la polisi Kanda maalumu ya Tarime na Rorya imethibitisha askari wake kumuua raia huyo, bila kutaja sababu ya mauaji hayo.
Hata hivyo, baada ya vuta nikuvute hiyo iliyodumu takribani dakika 45, hatimaye polisi walifanikiwa kuuchukuwa mwili huo wa marehemu Chacha na kuuondoa nao hospitalini hapo ukiwa chini ya ulinzi mkali wa polisi, na kwamba magari yaliyokuwepo eneo hilo yakiwa yamesheheni askari ni PT 2036, PT 1873, PT 1863, T 754 BLF pamoja na pikipiki moja ya doria, huku gari la halmashauri ya wilaya hiyo SM 5241 ndilo lililotumika kuubeba mwili huo wa marehemu.
Taarifa ya jeshi la polisi Kanda hiyo maalumu, iliyotolewa na Kaimu Kamanda wa Kanda hiyo ya Kipolisi, Sebastian Zacharia-SSP ilieleza kwamba awali marehemu alijeruhiwa kwa risasi tumboni na askari polisi, kwa madai ya kumkata panga mguu wa kushoto mlinzi mmoja wa mgodi huo, Winchlaus Petro (26).
“Kabla mauti kumkuta alijeruhiwa kwa kupigwa risasi tumboni na askari polisi waliokuwa doria eneo hilo la mgodi. Marehemu alianza kumshambulia askari kwa panga na kuikata silaha ya askari huyo mara mbili hata baada ya kuonywa kwa kupiga risasi hewani wakati wa kukamatwa”, ilisema sehemu ya taarifa hiyo ya polisi yenye kurasa moja.
Mganga Mfawidhi wa hospitali hiyo ya wilaya ya Tarime, Nagga Marco ilisema, uchunguzi wake umebaini marehemu Chacha alipigwa risasi ubavuni karibu na mgongo, kisha risasi hiyo ikatokea tumboni.
Kwa upande wao familia na ndugu wa marehemu huyo, akiwemo baba yake mkubwa, Charles Matiko waliieleza FikraPevu kwamba, nguvu iliyotumiwa na polisi kuchukuwa mwili wa kijana wao ni ya kinyama, kwani familia ilikuwa haijaridhia kuchukuliwa kwa marehemu kutokana na ukweli kwamba mipango ya maziko ilikuwa haijakamilika.
Mauaji ya watu eneo hilo la mgodi wa Nyamongo, yanaelezwa kushamiri, ambapo inadaiwa mwaka jana vijana wapatao watano waliuawa kwa kupigwa risasi na polisi, Mei 7 mwaka huu kijana mwingine aliyetajwa kwa jina moja la Mwikwabe aliauawa eneo hilo la mgodi, na kwamba Juni 4 mwaka huu marehemu Chacha aliuawa pia kwa kupigwa risasi ya moto na askari polisi wanaolinda mgodi huo wa North Mara ambao unamilikiwa na kampuni ya kigeni ya Barrick.
SOURCE;Jamii Forums
Habari imeandaliwa na Sitta Tuma, Tarime

Sunday, June 3, 2012

DIGITAL VIBES-STUDIO YA KISASA ZAIDI NDANI YA MOROGORO

eridelicious ndani ya Digital Vibes

                                                    Gq and Reyd

                                            Baadhi ya vifaa ndani ya studio hio

Thursday, May 10, 2012

TANESCO yaisamehe Zanzibar deni la bilioni 50/-

Default TANESCO yaisamehe Zanzibar deni la bilioni 50/-

WAKATI Shirika la Umeme Zanzibar (ZECO) likipandisha bei ya umeme kwa matumizi ya kawaida kwa wananchi kwa asilimia 40, imethibitika kwamba limefutiwa deni lake la muda mrefu kwa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO), linalofikia zaidi ya Sh bilioni 50.

Meneja Mkuu wa Zeco Hassan Ali Mbarouk alithibitisha kufutwa kwa deni hilo alipokutana na waandishi wa habari jana na kusema hali hiyo inatokana na ushirikiano mzuri kati ya pande mbili za Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Mbarouk alisema deni hilo lilifutwa baada ya uongozi wa shirika hilo kuwasilisha malalamiko yake ya muda mrefu na baadaye kukutana na aliyekuwa Waziri wa Nishati na Madini, William Ngeleja, na kupitia malalamiko yote na kuonekana kwamba deni hilo halina uhalali wa kuwapo.

Uongozi wa Zeco ulikuwa ukipinga ongezeko la bei ya umeme ambayo iliongezwa mwaka 2008.

“Tunamshukuru sana Waziri aliyekuwepo wakati ule (Ngeleja), alikutanisha pande mbili, Tanesco na Zeco na kusikiliza malalamiko na alikubaliana nasi na kutaka kufutwa kwa deni hilo kabla ya kuingizwa katika kero za Muungano,” alisema Mbarouk.

Alifafanua kuwa tatizo hilo limepatiwa ufumbuzi wa kudumu na sasa Zeco imekuwa ikilipa umeme inaonunua Tanzania Bara kwa awamu, lakini hawana deni linalotokana na malimbikizo au kubambikiziwa.

“Tunalo deni la kawaida tu kutoka kwa Tanesco la kununua umeme…hatuna deni linalotokana na utata wa kubambikiziwa,” alieleza Meneja huyo. Mapema, Shirika la Umeme Zanzibar lilieleza kwamba lipo katika hatua ya kutekeleza miradi miwili ya kuongeza vituo vya kusambaza umeme Unguja na kufadhiliwa na Serikali ya Japan.

Mradi unaofadhiliwa na Serikali ya Japan ni kwa ajili ya kujenga vituo vitatu vya kusambaza umeme kikiwamo cha Mpendae ambacho kitakuwa kikisambaza umeme katika ukanda wa Uwanja wa Ndege na Chukwani ambayo imekuwa ikikabiliwa na tatizo la kuzidiwa nguvu.

Meneja huyo wa Zeco alisema bado wanaendelea na mikakati ya kutafuta wawekezaji katika miradi ya umeme mbadala kwa lengo la kuhakikisha umeme wa uhakika unapatikana.

Source: Habari leo

My Take: Inasamehe madeni wakati yenyewe kila siku inalia njaa na kukopa mabilioni katika mabenki

Utengenezaji wa video mpya ya Chris Brown-Till i die

wiz khalifa,,Big Sean na Chris Brown
 Chris hakujiangala wakti anapiga picha au ndo swaga jinsi alivyovaa mkanda na suruali yake?


Facebook kuweka “Listen button” ya Muziki kwaajili ya Wanamuziki, Wasanii na Makampuni

10th May 2012 Blog 0
Muziki ni moja kati ya vitu muhimu vinavyo tufanya tuweze kutuliza mawazo ya hapa na pale, wakati huo huo kutupatia burudani ya pamoja na marafiki zetu. Iwe ni kwenye concet, klabu, barabarani ukiwa kwenye Daladala, Bajaji au kutoka kwenye simu yako. Lakini hususani tunapenda kusikiliza na kucheza muziki tukiwa pamoja na marafiki. Sasa inakuaje pale ambapo upo kazini, shuleni au nyumabi mwenyewe?
Sasa kwa kutumia account yako ya Facebook unaweza kusikiliza muziki unao upenda wewe pamoja na marafiki zako, na pia unaweza kusikiliza muziki kwa pamoja na Group members wako wa facebook. Kila mtu anaweza akawa DJ kwa marafiki zake na ukajihisi mpo pamoja siku nzima.
JINSI ITAKAVYO FANYA KAZI
Ili kuweza kusikiliza muziki anaosikiliza rafiki yako, Nenda kwenye ile sehemu yaku-Chart (chat sidebar) alafu angalia wale rafiki zako walioko online kwa wakati huo, hivyo kwa wale marafiki zako amabo watakua tayari wanatumia hiyo application ya muziki live kwa facebook yao, itakupa fursa ya wewe ku+Click na kuweza kusikiliza mziki huo, pia hapo hapo kwa hilo group la muziki mnaosikiliza mtaweza ku+Chat wote kwa pamoja na kumwambia DJ wenu aweze kuwapa/ kuwasikilizisha muziki muupendao. Hivyo Rafiki yenu sasa anakua DJ wenu, kwakua anajua mnachokipenda.
Listen button Inavyoonekana wakati unataka kuchagua usikilize muziki wa nanai | PICTURE SOURCE: Facebook Blog
JINSI YA KUJISAJILI KUWA DJ
Sasa unaweza kwenda Turntable.fm | Spotify, Myspace au OMG na kujisajili kama mtumiaji, ili Facebook watakapo izindua hivi karibuni (Mwishoni mwa mwezi huu wa April) uwe tayari umesajiliwa na kuweza kuwaburudisha marafiki zako wote unaowapenda.
JE INA FAIDA GANI KWA WANAMUZIKI WETU TANZANIA?
Wanamuziki wetu wa hapa Nchini Tanzania na East Africa kwa Ujumla, wataweza kuweka “Listen Button” kwenye Fan Page zao, na kuwawezesha wapenzi wao wa muziki kuingia na kuwasikiliza moja kwa moja wakiwa Facebook, na kuwafanya kuweza kuelewa ni nyimbo gani haswa hupendwa na Mashabiki zao.
Mfano wa FanPage hizo kwaajili ya wanamuziki na wasanii kwa ujumla utakua kama unavyoonekana kwenye picha hii hapa chini ambapo “Listen button” itakua hapo chini kulia pembeni mwa Likes.

Mfano wa Jinsi Fanpage ya MwanaFa Inavyoonekana akiwa Msanii wa Kwanza Tanzania Kupata Listen Button Ikiwa Kwenye Majaribio
Ni Muda muafaka sasa kwa wasanii na wanamuziki wetu wa Tanzania kutumia fursa hii kuufanya muziki wako kua Social, ambapo watapata maoni zaidi kutoka kwa mashabiki wao na wakati huo huo kuweza kuboresha kazi zao. Hivyo kuwaongezea wanamuziki na wasanii wote kwa ujumla, kuzidi kupendwa zidi na Fans wao hivyo kuwasaidia kuuza vitu vyao malimbali kama picha, cd, t-shirts, Concert tickets na vitu vingine ambavyo vitawaingizia mapato kutokana na Fans wao.
Sasa unaweza kusikiliza muziki uupendao popote ukiwa online pamoja na marafiki zako
Kwa Msaada Wa PopoteMedia
 mx

Wednesday, May 9, 2012

HIGH VOLTAGE: Mwingereza matatani kwa ugaidi K...

HIGH VOLTAGE: Mwingereza matatani kwa ugaidi K...: Mwingereza matatani kwa ugaidi Kenya  9 Mei, 2012 - Saa 10:29 GMT ...

Mwingereza matatani kwa ugaidi Kenya

 9 Mei, 2012 - Saa 10:29 GMT
Jermain Grant
Raia wa Uingereza ambaye ni mwislamu na mwenye msimamo mkali amefikishwa katika mahakama moja mjini Mombasa, Kenya .
Jermaine Grant mwenye umri wa miaka 29 , alitiwa mbaroni mwezi Disemba mwaka jana kwa tuhuma za kupanga mashambulizi ya bomu pamoja na kumiliki vilipuzi kinyume cha sheria.
Maafisa wa serikali ya Kenya wanasema raia huyo kutoka London, ana uhusiano na kundi la wapiganaji la Al Shabab nchini Somalia, ambaye pia aliwahi kufungwa nchini humo kwa kutokuwa na kibali cha kuingia nchini.
Anashtakiwa pamoja na wenzake watatu ambao ni raia wa Kenya ambapo amekana tuhuma zinazomkabili.
Mwandishi wa BBC aliyepo Mombasa Gabriel Gatehouse ,anasema Grant amefika mahakamani akiwa ametulia.
Waandishi wa habari walifurika katika mahakama hiyo na haikujilikana kama kesi hiyo inaweza kuendelea.
Inaarifiwa kesi yenyewe ingali inakumbwa na utata.
Grant alitiwa mbaroni kwa mara ya kwanza mwaka 2008 katika eneo la mpaka waKenya na Somalia lakini alitoroka wakati alipokuwa mahabusu katika kituo cha polisi.
Duru zinaarifu mtuhumiwa alitoroshwa kutoka kituo cha polisi na kundi la Al Shabab.

Saturday, May 5, 2012

TODAY'S BEAUTIFUL QOUTES

The most beautiful thing we can experience is the mysterious. It is the source of all true art and science.
Albert Einstein

Joy in looking and comprehending is nature's most beautiful gift.
Albert Einstein

However beautiful the strategy, you should occasionally look at the results.
Winston Churchill

For beautiful eyes, look for the good in others; for beautiful lips, speak only words of kindness; and for poise, walk with the knowledge that you are never alone.
Audrey Hepburn

It is better to be beautiful than to be good. But... it is better to be good than to be ugly.
Oscar Wilde

No object is so beautiful that, under certain conditions, it will not look ugly.
Oscar Wilde

When you're a carpenter making a beautiful chest of drawers, you're not going to use a piece of plywood on the back, even though it faces the wall and nobody will ever see it. You'll know it's there, so you're going to use a beautiful piece of wood on the back.
Steve Jobs

I knew I belonged to the public and to the world, not because I was talented or even beautiful, but because I had never belonged to anything or anyone else.
Marilyn Monroe

Nothing is beautiful, only man: on this piece of naivete rests all aesthetics, it is the first truth of aesthetics. Let us immediately add its second: nothing is ugly but degenerate man - the domain of aesthetic judgment is therewith defined.

Rais Jakaya Mrisho Kikwete,kwa mujibu wa madaraka ya kikatiba aliyonayo,hivi leo ametangaza Baraza La Mawaziri. Hii hapa chini ni orodha kamili ya Baraza hilo likijumuisha Mawaziri na Manaibu Waziri ambayo kimsingi ina majina takribani yale yale ya Baraza La Mawaziri lililopita isipokuwa machache na pia mabadiliko ya majina fulani kutoka Wizara moja hadi nyingine.
Shughuli ya kuliapisha Baraza hili inatarajiwa kufanyika Jumatatu tarehe 7/5/2012 Ikulu jijini Dar-es-salaam.

OFISI YA RAIS
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Mahusiano na Uratibu)
Ndugu Stephen M. Wasira, Mb.,
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, (Utawala Bora)
Ndugu George Mkuchika, Mb.,
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (UTUMISHI)
Ndugu Celina Kombani, Mb.,

OFISI YA MAKAMU WA RAIS
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (MUUNGANO)
Ndugu Samia H.  Suluhu, Mb.,
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (MAZINGIRA)
Dr. Terezya P.L. Huvisa, Mb.,

OFISI  YA WAZIRI MKUU
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri  Mkuu (Uwekezaji na Uwezeshaji)
Ndugu Mary M. Nagu, Mb.,
Waziri wa Nchi, Ofisi  ya Waziri Mkuu (TAMISEMI)
Ndugu Hawa Ghasia, Mb.,
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Bunge)
Ndugu William V. Lukuvi, Mb.,

WIZARA
Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki- Ndugu Samuel J. Sitta, Mb.,
Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa- Ndugu Shamsi Vuai Nahodha, Mb.,
Waziri wa Ujenzi- Dr.  John P. Magufuli, Mb.,
Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii- Dr. Hussein A.H. Mwinyi, Mb.,
Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi-Dr. Shukuru J. Kawambwa, Mb.,
Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto-Ndugu Sophia M. Simba, Mb.,
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa-Ndugu Bernard K. Membe, Mb.,
Waziri wa Katiba na Sheria -Ndugu Mathias M. Chikawe, Mb.,
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi-Ndugu Emmanuel Nchimbi, Mb.,
Waziri wa Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi-Dr. David M. David, Mb.,
Waziri wa Kazi na Ajira -Ndugu Gaudentia M. Kabaka, Mb.,
Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia-Prof.  Makame M. Mbarawa, Mb.,
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi -Prof.  Anna K. Tibaijuka, Mb.,
Waziri wa Maji-Prof. Jumanne Maghembe,  Mb.,
Waziri asiyekuwa na Wizara Maalum-Prof. Mark Mwandosya, Mb.,
Waziri wa  Kilimo, Chakula na Ushirika-Eng. Christopher Chiza, Mb.,
Waziri wa Uchukuzi -Dr. Harrison Mwakyembe, Mb.,
Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo-Dr. Fenella E. Mukangara, Mb.,
Waziri wa Maliasili na Utalii-Ndugu Khamis Kagasheki, Mb.,
Waziri wa Viwanda na Biashara -Dr. Abdallah O. Kigoda, Mb.,
Waziri wa Fedha-Dr. William Mgimwa, Mb.,
Waziri wa Nishati na Madini-Prof. Sospeter Muhongo, Mb.,

NAIBU MAWAZIRI
OFISI YA RAIS
HAKUNA NAIBU WAZIRI
OFISI YA MAKAMU WA RAIS
Naibu Waziri, Ofisi ya Makamu wa Rais
Ndugu Charles Kitwanga, Mb.,

OFISI YA WAZIRI MKUU
Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi  ya Waziri Mkuu (TAMISEMI)- Ndugu Majaliwa K. Majaliwa, Mb.,
Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi  ya Waziri Mkuu (TAMISEMI)-Ndugu Aggrey Mwanry, Mb.,
WIZARA MBALIMBALI
Naibu Waziri wa Kazi na Ajira-Dr. Makongoro M. Mahanga, Mb.,
Naibu Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika-Ndugu Adam Malima, Mb.,
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi-Ndugu Pereira A. Silima, Mb.,
Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara-Ndugu Gregory G. Teu, Mb.,
Naibu Waziri wa Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi-Ndugu Benedict N. Ole-Nangoro, Mb.,
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa-Ndugu Mahadhi J. Maalim, Mb.,
Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo  ya Makazi,-Ndugu Goodluck J. Ole-Medeye, Mb.,
Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto -Ndugu Ummy A. Mwalimu, Mb.,
Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi -Ndugu Philipo A. Mulugo, Mb.,
Naibu Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki -Dr. Abdulla Juma Abdulla, Mb.,
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii-Ndugu Lazaro Nyalandu, Mb.,
Naibu Waziri wa Ujenzi-Ndugu Gerson Lwenge,Mb.,
Naibu Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii,-Dr. Seif Suleiman Rashid,Mb.,
Naibu Waziri wa Nishati na Madini-Ndugu George Simbachawene, Mb.,
Naibu Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia-Ndugu January Makamba, Mb.,
Naibu Waziri wa Uchukuzi-Dr. Charles J. Tizeba, Mb.,
Naibu Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo-Ndugu Amos Makala, Mb.,
Naibu Waziri wa Maji-Eng. Dr. Binilith Mahenge,Mb.,
Naibu Waziri Nishati na Madini-Ndugu Stephen Maselle, Mb.,
Naibu Waziri wa Katiba na Sheria-Ndugu Angela Jasmine Kairuki, Mb.,
Naibu Waziri wa Fedha-Ndugu Janet Mbene, Mb.,
Naibu Waziri wa Fedha-Ndugu Saada Mkuya Salum, Mb.,

Read more: BARAZA LA MAWAZIRI TANZANIA AS ANNOUNCED ON MAY 4th 2012 - BongoCelebrity

Friday, May 4, 2012

BARAZA LA ZAMANI LA MAWAZIRI,,


The Cabinet

Portfolio Name
President and Commander -in- Chief of the Armed Forces of the United Republic of Tanzania H.E Jakaya Mrisho Kikwete
Vice - President H.E Dr. Mohamed Gharib Bilal 
President of Zanzibar H.E Dr. Ali Mohamed Shein  
Prime Minister of the United Republic of Tanzania Hon. Mizengo Kayanza Peter Pinda  
Ministers of State in the President's Office  
     Public Service Management Hon. Hawa Abdulrahman Ghasia
     Good Governance
Hon. Mathias Meinrad Chikawe
     Social Relations and Co-ordination
Hon. Stephen Masatu Wassira
Ministers of State in the Vice President's Office
     Union Affairs Hon. Samia Suluhu
     Environment Hon. Terezya Hoviza

Ministers of State in the Prime Minister's Office  

     Regional Administration and Local Government Hon. George Mkuchika
     Policy, Co-ordination and Parliamentary Affairs Hon. William Lukuvi
     Investiment and Empowerment Hon. Dr. Mary Michael Nagu
Minister for Foreign Affairs and International Co-operation Hon. Bernard Kamillius Membe
Minister for East African Co-operation Hon. Samwel John Sitta
Minister for Finance Hon. Mustafa Mkulo 
Minister for Industry, Trade and Marketing Hon. Dr. Cyril Chami
Minister for Agriculture, Food Security and Co-operatives Hon. Prof. Jumanne Abdallah Maghembe
Minister for Natural Resources and Tourism Hon. Ezekiel Maige
Minister for Water Hon. Prof. Mark James Mwandosya
Minister for Energy and Minerals Hon. William Ngeleja
Minister for Works Hon. Dr. John Pombe Joseph Magufuli
Minister for Transport Hon. Omary Nundu
Minister for Communication, Science and Technology Hon. Prof. Makame Mnyaa Mbarawa
Minister for Health and Social Welfare Hon. Dr. Haji Hussein Mpanda
Minister for Education and Vocational Training Hon. Dr. Shukuru Jumanne Kawambwa
Minister for Labour and Employment Hon. Gaudensia Mugosi Kabaka
Minister for Lands, Housing and Human Settlements Development Hon. Prof. Anna Tibaijuka
Minister for Information, Youth, Culture and Sports Hon. Dr. Emmanuel John Nchimbi
Minister for Defence and National Service Hon. Dr. Hussein Ali Mwinyi
Minister for Home Affairs Hon. Shamsi Vuai Nahodha
Minister for Justice and Constitutional Affairs Hon. Celina Ompeshi Kombani
Minister for Community Development, Gender and Children Hon. Sofia Mnyambi Simba
Minister for Livestock and Fisheries Development   Hon. Mathayo David Mathayo



Deputy Ministers and Their Respective Ministries
 
Prime Minister’s Office
Regional Administration and Local Government  
  • Hon. Aggrey Mwanri
  • Hon. Kassim Majaliwa
Foreign Affairs and International Co-operation Hon. Mahadhi Juma Mahadhi
East African Co-operation Hon. Dr Abdallah Juma Abdallah
Finance  
  • Hon. Gregory Teu
  • Hon. Pereira Ame Silima
Industry, Trade and Marketing Hon. Lazaro Nyalandu
Agriculture, Food Security and Co-operatives Hon. Eng. Christopher Chiza
Energy and Minerals Hon. Adam Malima
Works
Hon. Harrison Mwakyembe
Transport
Hon. Athumani Mfutakamba
Communication, Science and Technology Hon. Charles Kitwanga
Health and Social Welfare Hon. Lucy Nkya
Education and Vocational Training Hon. Philipo Mulugo
Labour and Employment Hon . Makongoro Mahanga
Community Development, Gender and Children Hon. Umi Ali Mwalimu
Home Affairs Hon. Khamis Sued Kagasheki
Livestock ang Fisheries Development Hon. Benedict Ole Nangoro
Natural Resources and Tourism -
Water Hon. Eng. Gerson Lwinge
Information, Youth, Culture and Sports Hon. Dr. Fenella Mukangara
Defence and National Service -
Nafikiri unahitaji kunifahamu japo hata kwa picture

Monday, April 30, 2012

MY BLOG

1 of May 2012,i just opened my on blog,,it is just a beginning