Facebook kuweka “Listen button” ya Muziki kwaajili ya Wanamuziki, Wasanii na Makampuni
Sasa kwa kutumia account yako ya Facebook unaweza kusikiliza muziki unao upenda wewe pamoja na marafiki zako, na pia unaweza kusikiliza muziki kwa pamoja na Group members wako wa facebook. Kila mtu anaweza akawa DJ kwa marafiki zake na ukajihisi mpo pamoja siku nzima.
JINSI ITAKAVYO FANYA KAZI
Ili kuweza kusikiliza muziki anaosikiliza rafiki yako, Nenda kwenye ile sehemu yaku-Chart (chat sidebar) alafu angalia wale rafiki zako walioko online kwa wakati huo, hivyo kwa wale marafiki zako amabo watakua tayari wanatumia hiyo application ya muziki live kwa facebook yao, itakupa fursa ya wewe ku+Click na kuweza kusikiliza mziki huo, pia hapo hapo kwa hilo group la muziki mnaosikiliza mtaweza ku+Chat wote kwa pamoja na kumwambia DJ wenu aweze kuwapa/ kuwasikilizisha muziki muupendao. Hivyo Rafiki yenu sasa anakua DJ wenu, kwakua anajua mnachokipenda.
Listen button Inavyoonekana wakati unataka kuchagua usikilize muziki wa nanai | PICTURE SOURCE: Facebook BlogSasa unaweza kwenda Turntable.fm | Spotify, Myspace au OMG na kujisajili kama mtumiaji, ili Facebook watakapo izindua hivi karibuni (Mwishoni mwa mwezi huu wa April) uwe tayari umesajiliwa na kuweza kuwaburudisha marafiki zako wote unaowapenda.
JE INA FAIDA GANI KWA WANAMUZIKI WETU TANZANIA?
Wanamuziki wetu wa hapa Nchini Tanzania na East Africa kwa Ujumla, wataweza kuweka “Listen Button” kwenye Fan Page zao, na kuwawezesha wapenzi wao wa muziki kuingia na kuwasikiliza moja kwa moja wakiwa Facebook, na kuwafanya kuweza kuelewa ni nyimbo gani haswa hupendwa na Mashabiki zao.
Mfano wa FanPage hizo kwaajili ya wanamuziki na wasanii kwa ujumla utakua kama unavyoonekana kwenye picha hii hapa chini ambapo “Listen button” itakua hapo chini kulia pembeni mwa Likes.

Mfano wa Jinsi Fanpage ya MwanaFa Inavyoonekana akiwa Msanii wa Kwanza Tanzania Kupata Listen Button Ikiwa Kwenye Majaribio
Sasa unaweza kusikiliza muziki uupendao popote ukiwa online pamoja na marafiki zako
Kwa Msaada Wa PopoteMedia
mx
No comments:
Post a Comment